Pate

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya kisiwa cha Pate (Kenya)

Pate ni kisiwa kikubwa cha funguvisiwa la Lamu mbele ya pwani ya Kenya katika Bahari Hindi. Pate ni kisiwa ambacho ni karibu na Somalia.

Wakati ya maji kujaa Pate inagawanywa katika sehemu mbili kwa mtaro wa bahari karibu na Siyu; wakati wa maji kupwa mtaro huwa pakavu.

Pate ilikuwa kati ya mahali pa kwanza kutembelewa na wafanyabiashara Waarabu, labda kuanzia karne ya 7 BK. Inawezekana ilikuwa tayari kati ya mahali palipotajwa katika taarifa za kale kuhusu Azania kama vile Periplus ya Bahari ya Eritrea.

Kisiwa cha Pate kilikuwa mahali pa miji muhimu ya Waswahili Pate, Siyu na Faza iliyoshindana na mji wa Lamu juu ya kipaumbele katika funguvisiwa.

Katika karne ya 19 umuhimu wa miji hiyo ilirudi nyuma na kisiwa kilikuwa sehemu ya dola la Usultani wa Zanzibar.

Siku hizi Faza ni kijiji kikubwa cha Pate chenye hospitali ndogo, polisi, nyumba ya wageni, shule ya sekondari na maduka.

Mwaka 2004 palikuwa na gari moja tu kisiwani, yaani gari la hospitali.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Boteler, Thomas (1835). Narrative of a Voyage of Discovery to Africa and Arabia: performed in His Majesty´s ship Leven and Barracouta from 1821 to 1826. Juz. 1. R. Bentley. Iliwekwa mnamo 10 Desemba 2013.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  • Burton, Richard Francis (1872). Zanzibar: city, island, and coast. Juz. 2. London: Tinsley brothers.
  • Martin, Chryssee MacCasler Perry and Esmond Bradley Martin: Quest for the Past. An historical guide to the Lamu Archipelago. 1973.
  • Mark Horton; with contributions by Helen W. Brown and Nina Mudida: Shanga: the archaeology of a Muslim trading community on the coast of East Africa. Memoirs of the British Institute in Eastern Africa; No. 14 London: British Institute in Eastern Africa, 1996. ISBN 1-872566-09-X

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]