Mkata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mkata ni kata ya Wilaya ya Handeni Vijijini katika Mkoa wa Tanga, Tanzania.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 40,365 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 31,879 waishio humo.

Upande wa makabila, wakazi wengi ni Wazigua ambao walianza kuishi humo toka zama za ukoloni, na wengi wao ni Waislamu.

Wakazi wengi hutegemea kilimo na biashara ndogondogo. Pia Mkata huongoza kwa uuzwaji wa nyamachoma za mbuzi.

Kata ya Mkata kwa muda mwingi ilikuwa na changamoto ya maji, ila alipoingia madarakani Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa awamu ya 5, akafanikiwa kutatua tatizo hilo kwa kuweka mabomba ya maji nyumbani mwa watu, ijapokuwa mabwawa yamekauka na hali ya maji kuwa ya kusuasua.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Handeni Vijijini - Mkoa wa Tanga - Tanzania

Kabuku | Kabuku Ndani | Kang'ata | Kitumbi | Kiva | Komkonga | Kwachaga | Kwaluguru | Kwamatuku | Kwamgwe | Kwamsisi | Kwankonje | Kwasunga | Kwedizinga | Mazingara | Mgambo | Misima | Mkata | Ndolwa | Segera | Sindeni

Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Tanga bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkata kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.