Maroni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha ya Kirusi ya Mt. Maroni.

Maroni (kwa Kiaramu ܡܪܝ ܡܪܘܢ, Mar|Mār(y) Mārōn; kwa Kiarabu: مار مارون‎) alikuwa padri mkaapweke mwenye juhudi za sala, lakini pia za umisionari nchini Siria.

Alifariki kati ya mwaka 406 na mwaka 423 akaanza mara kuheshimiwa kama mtakatifu. Wakristo wengi walihamia kwenye kaburi lake na ndio mwanzo wa tapo la kiroho lenye jina lake ambalo lilizaa nchini Lebanon Kanisa la Wamaroni lililomo katika ushirika kamili na Kanisa la Roma na Kanisa Katoliki lote duniani.

Kuanzia karne ya 17, sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 9 Februari[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.